Nimechoka Poem by Abdallah Mpogole

Nimechoka

Rating: 3.0

Sikuipenda dunia niliyoishi,
Na sikupenda vile nilivyoishi.

Dunia ilo na Jua na kila aina ya nuksi,
Watu waso na kauli, Vinywani mwao matusi.

Hakika Siamini kama naweza endelea kuishi.

Nimeishi sana nimechoka,
Natamani muda huu kuondoka.

Niende mbali kule nisikofika,
palo ugumu kushika na paso sikika.

Utanikosa japo mawazoni sintokutoka,
Usisononeke na iwapo wantaka,

Jitahidi kulala na ipo siku njozini utaniota.

COMMENTS OF THE POEM
READ THIS POEM IN OTHER LANGUAGES
Abdallah Mpogole

Abdallah Mpogole

Iringa, Tanzania
Close
Error Success